Ijumaa, 15 Machi 2013

HUKU NAPO SIPO

WAZIRI ACHARUKIA SKENDO YA JACK CHUZ KUJIUZA

Stori: Gladness Mallya na  Hamida Hassan
BAADA ya hivi karibuni msanii wa filamu, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ kunaswa akipelekwa kuuzwa kwa mwanaume, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla anadaiwa kuicharukia skendo hiyo ambapo juzikati alimvaa Rais wa Shirikisho la Filamu (TAFF), Simon Mwakifwamba na kumuuliza juu ya tukio hilo la aibu.
Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’.
Chanzo cha habari kutoka ndani ya shirikisho hilo kililitonya Ijumaa kuwa, Mhe. Makalla alimvaa Mwakifwamba kwenye mkutano na wasanii uliofanyika ndani ya Hoteli ya Kibadamu, Ubungo jijini Dar.
“Mhe. Makalla ndiye aliyekuwa mgeni rasmi, akiwa pale alimuuliza Mwakifwamba kuhusu hatua walizochukua kwa Jack Chuzi baada ya kuandikwa habari kuwa alinaswa akienda kuuzwa.
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla.
“Mwakifwamba alijitetea kuwa, wanalishugulikia na Mwenyekiti wa Chama cha Waigizaji Tanzania, Michael Sangu ‘Mike’ akasisitiza kuwa, wako katika mchakato wa kulitolea uamuzi tukio hilo lililofanywa na Jack ,” kilidai chanzo hicho.
Baada ya kuzinyaka habari hizi paparazi wetu alimtafuta Mwakifwamba lakini hakuweza kupatikana mara moja ila Mike alipoulizwa juu taarifa za Mhe. Makalla kucharukia ishu ya Jack alisema:
Rais wa Shirikisho la Filamu (TAFF), Simon Mwakifwamba.
“Ni kweli waziri aliuliza kuhusu hatua tulizozichukua kuhusu suala la Jack kujiuza ambapo nilimjibu kuwa tuko kwenye mchakato wa kulitolea uamuzi na kwa sasa tumeunda kamati maalum, ikimaliza uchunguzi wake ndiyo tutatoa jibu kuwa tumemchukulia hatua gani.”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni