Ijumaa, 8 Machi 2013

JIANDAE NA..


Maonyesho ya filamu za Afrika yaanza

 09march, 2013 - Saa 16:41 GMT

Tuzo ya Stallion of Yennenga inayotolewa kwenye maonyesho ya Ouagadougou
Maonyesho ya filamu mia kadha kutoka sehemu mbali-mbali za Afrika na Wafrika walioko ng'ambo, zitaoneshwa katika tamasha kubwa ya utamaduni wa Afrika ambayo inaanza Burkina Faso Jumamosi.
Maonyesho hayo ya Panafrican Film and Television Festival ya Ouagadougou (FESPACO) yanafanywa kila baada ya miaka miwili.
Tuzo kubwa kabisa - Stallion of Yennenga - hupewa filamu ambayo inaonesha maisha halisi kabisa ya Afrika.
Filamu 20 za habari hasa kutoka Morocco, Algeria, Angola na Senegal zinagombea tuzo hiyo.
Ingawa Misri haikujiandikisha kwenye mashindano hata hivyo itaonesha filamu ya msanii wa Misri, Khaled Sayed, iitwayo "Stories from Tahrir".
Inaangalia changamoto ambazo Wamisri wanakabili wanapogombania uhuru.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni